Dr mlelwa Lectures
Ni darasa la kimtandao lililo anza mnamo mwaka 2020 na Mtumishi Helbeth Mlelwa( Dr Mlelwa) na kuungana na Eng Anold Amri mwaka huo huo
Kwa mawasiliano:-
Dr mlelwa official: 0745965125 au 0714483548
Eng Anold amri :0693662424
Dr Mlelwa amekuwa mwanafunzi chuo kikuu cha MUHAS na alikuwa Tanzania One (TO) katika somo la biology mwaka 2018 na baadaye akaja
na wazo hili la kuanza kufunsha wanafunzi wengi zaidi kwa njia ya mtandao hata wale walio mbali naye.
Eng Anold Amri ni mwanafunzi wa MUST(Mbeya university of science and technology) akisoma kozi ya BACHEROL IN COMPUTER ENGINEERING
na ndiye aliye tengeneza hii website na kuhakikisha inawasaidia na kuwanufahisha watanzania.
Sisi tumejipanga kuhakikisha wanafunzi wote tanzania wanakuwa na wepesi katika safari yao ya masomo lakini pia tunatoa fulsa kwa
watu walio na ujuzi mwingine kuuza katika tovuti hii ili wanafunzi pia wawe na ujuzi nje na masomo wanayosoma utakao wasaidia wao
kujipatia kipato baada ya kujifunza ujuzi huo pia itasaidia kutatua matatizo katika jamii wanazoishi.
Malengo yetu ni kuja kuwa na wanafuzi zaidi ya elfu 50 wnaotumia website yetu ili kuinua ufaulu wa wanafunzi na kutatua changamoto
ya mwanafunzi kushindwa kufaulu kwa sababu ya kukosa mwalimu shuleni kwao, ndio maana bei ya vipindi vyetu ni bei inayoweza kulipwa na
kila mtanzania.
Tumejipanga kuhakikisha kuwa kila mwalimu atakaye fundisha ujuzi wowote kupitia website hii basi atoe ujuzi huo katika ubora na usahihi
ili kujenga taifa lenye wasomi tija katika jamii na familia zetu.
Mwisho ni kwamba sisi dr Mlelwa tunaamini katika Mungu yaani tunaamini BIBILI NA KURUANI takatifu ni vitabu vya Mungu na vinahimiza wema
na utu kwa watu wote, hivyo tunaamini katika vitabu hivi tu na kufanya ibada, swala na kuomba Mungu siku zote hatuamini katika matusi,
elevi, uzinzi na wizi kama tunavyo amliwa katika vitabu hivyo vitakatifu.
Write a public review